HABARI MPYA
blink

KENYA YAZINDUA UJENZI WA RELI KUELEKEA UGANDA NA RWANDA

Written By Unknown on Jumamosi, 30 Novemba 2013 | 18:09


Kenya imezindua rasmi ujenzi wa njia ya Reli itakayounganisha kanda ya Afrika Mashariki na eneo la maziwa makuu ujenzi utakaofadhiliwa na serikali ya China.
Reli hiyo itaunganisha Kenya na Sudan Kusini, DR Congo na Burundi.
Sehemu ya kwanza ya njia hiyo ya reli , itaunganisha bandari ya Mombasa na Mji mkuu Nairobi na kupunguza muda wa safari kati ya miji hiyo kutoka masaa 15 hadi masaa manne tu.
Huu bila shaka ndio utakuwa mradi mkubwa Zaidi kuwahi kujengwa tangu nchi hiyo kujipatia uhuru miaka 50 iliyopita.
Mradi huo utagharimu dola bilioni 5.2 kiasi kikubwa cha pesa hizo kikitolewa na Uchina.

Baadhi ya wakenya wanalalamika kuwa tenda hiyo imetolewa kwa kampuni ya kichina kwa njia isiyofaa.
Rais Uhuru Kenyatta katika hafla ya uzinduzi huo amesema kuwa mradi huu ndio utakuwa kumbukumbu kubwa ya utawala wake Kenya.
Mkataba wa ujenzi wa njia hiyo ya reli, ulifikiwa kati ya Rais Kenyatta na mwenzake wa China Xi Jinping mnamo mwezi Agosti mjini Beijing.
Pia kuna matumaini kuwa njia hiyo ya reli itapunguza msongamano mjini Mombasa moja ya bandari yenye shughuli chungu nzima barani Afrika.
Njia ya reli iliyoko sasa, ni ile iliyojengwa enzi za ukoloni.
Baada ya kukamilika kwa sehemu ya kwanza ya reli hiyo mjini Nairobi, mwaka 2017, itaendelezwa hadi Magharibi mwa DRC hususan mjini Kisangani, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini.
"Tunachokifanya hapa leo, kitaleta mageuzi makubwa sio nchini Kenya tu bali katika kanda nzima ya Afrika Mashariki,’’ alisema Rais Kenyatta akitaja mradi huo kama jambo la kihistoria.
Aliongeza kusema kuwa mradi huu ni moja ya miradi mikubwa katika maono yake ya maendeleo itimiapo mwaka 2030 kuboresha hali ya miundo msingi nchini humo.

GAZETI LA MWANANCHI 30, NOV

HABARI KUU

Mishahara ya vigogo ‘hailingani na ufanisi’

Posted 15 hours ago
Ripoti mpya ya utafiti imebainisha kuwa mishahara mikubwa wanayolipwa viongozi wa juu serikalini na wanasiasa hailingani na utendaji wao wa kazi....

AFRIKA MASHARIKI NAYO KAMA ULAYA-SARAFU MOJA KUANZISHWA


Baada ya sintofahamu ya muda mrefu kuhusu jumuiya ya afrika mashariki kuwa na sarafu moja, hatimae wakubwa leo wanasaini mkataba wa sarafu moja ya afrika mashariki

Hatua hii inakuja huku kukiwa na vuguvugu la baadhi ya nchi kutaka kuzitenga nyingine katika harakati za ukuaji wa uchumi wa afrika mashariki pamoja mahusiano ya kisiasa miongoni mwao

Katibu mkuu wa jumuiya hiyo yenye makao makuu yake mkoani Arusha nchini Tanzania Bw. Richard Sezibera amekaririwa na vyombo vya habari mapema leo akieleza kuwa wakuu wan chi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wanasaini mkataba huo katika viwanja vya kilolo au Uhuru mjii Arusha

PANGUA PANGUA JESHI LA POLISI TANZANIA

IGP Said Mwema (Mkuu wa jeahi la Polisi Tanzania)

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema   amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera pamoja na baadhi ya Wakuu wa Upelelezi wa mikoa na  wakuu wa Polisi wa Wilaya katika baadhi ya mikoa hapa Nchini.

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Philipo Kalangi amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam, kuwa Mkuu  wa kikosi cha kusimamia usalama wa Mazingira na nafasi yake  inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) George Mayunga ambaye alikuwa Mkuu wa kikosi cha  kusimamia mazingira Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

 Aidha, baadhi ya Wakuu wa Upelelezi wa  mikoa (RCO) na wakuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) waliobadilishwa ni pamoja na 
aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa  makosa ya jinai mkoa wa Tabora ACP Edward Bukombe amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam, Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Geita (RCO) ACP Francis Kibona  amehamishiwa mkoa wa Njombe kuwa mkuu wa Upelelezi mkoa na  nafasi yake inachukuliwa na SSP Simon Pasua kutoka  Makao makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.

Wengine ni aliyekuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ya Wanging’ombe SSP. Francis Maro amehamishiwa Mkoa wa Katavi kuwa Mkuu wa upelelezi wa mkoa na aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoa wa Katavi ACP. Emmanuel Nley amehamishiwa kikosi cha Polisi wanamaji Dar es Salaam. Mkuu wa Upelelezi mkoa wa  Rukwa SSP. Peter Ngussa amehamishiwa Makao makuu ya Upelelezi Dar es Salaam, nafasi yake inachukuliwa na SSP  Alan Bukumbi aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Njombe.

Aliyekuwa Mkuu wa Polisi wilaya ya kati( OCD) Mrakibu wa  Polisi (SP) Salum Ndalama anaenda kuwa kaimu mkuu wa upelelezi mkoa wa Tabora na aliyekuwa mkuu wa Polisi wa  wilaya ya Tunduru (OCD) SP. Amadeus Tesha anakwenda kuwa Mkuu wa upelelezi kikosi cha Polisi reli.

Uhamisho huo ni wa kawaida katika kuboresha utendaji kwa  mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.

Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.


World AIDS Day 2013 Statement by Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group



PRESS RELEASE

World AIDS Day 2013 Statement by Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group

World AIDS Day is December 1

TUNIS, Tunisia, November 29, 2013-- Africa has made significant progress in fighting the HIV/AIDS pandemic. In the past seven years, AIDS-related deaths declined by 32%.The number of people contracting the HIV infection declined by 25% in the past 10 years. The rate of mother-to-child transmission of HIV has also declined from 35% in 2001 to 26% in 2010. Ten years ago, we had fewer than 50,000 people on ARV treatment; today we have over 6 million receiving treatment. A few years ago, Senegal and Uganda were the only success stories for their outstanding results and containment of HIV; now we have 25 countries that lowered HIV infections by more than 50%. A lot has been achieved; however, the risks are far from over. Indeed, new infections are a threat. It is time to raise, not to lower our vigilance.


Recall, 30 years ago, when the first HIV-positive case was reported; 24 million Africans have lost their lives. Africa still bears the heaviest burden of the disease globally and accounts for 91% of the world’s children with HIV, 89% of HIV orphans and 69% of people living with HIV. Each day, 3,500 Africans die of AIDS and millions of others and their families and communities go through economic, psychological and social traumas. HIV-related stigma still hurts people, in society, in their workplaces and homes. Women in Africa are more severely affected than men. In 2012, 58% of people living with HIV were women.

HIV/AIDS continues to have a huge detrimental impact on the most important resource of our continent: our people. It robs the continent of vitally needed skilled workers and deprives families of their incomes. It has hampered our ability to educate and build our human capital. Kenya lost an estimated 1.7% of its teachers between 2000 and 2010 due to HIV/AIDS.

For the African Development Bank, in partnership with governments, international organizations, civil society and the private sector, the future of HIV/AIDS agenda is about ‘getting to zero’. Zero new HIV infections, zero discrimination and zero AIDS-related deaths. Getting there is not easy and the Bank aims to support African countries to, first, take ownership of the AIDS response. It is time for Africa to take bold steps to reduce dependence on external donors and work towards more sustainable domestic solutions. According to UNAIDS, Africa will require between US $11 billion and $12 billion for its AIDS response by 2015. Yet international funding to HIV is dwindling, putting our progress at risk.

Second, the Bank supports African countries in increasingly applying ‘value for money’ and ‘solidarity’ principles to strengthen social systems. The way HIV resources are mobilized and spent needs to change. The vertical approach may no longer be appropriate and cost-effective in many contexts. There is a need to mainstream AIDS-related services into the general healthcare delivery systems and to support the local production of ARVs.

Third, the Bank supports the building of inclusive health systems to fight stigma and discrimination. Let us all tackle stigma and discrimination by building a supportive and caring culture both in their communities and workplaces. We cannot leave the victims of HIV/AIDS and their families behind.

Finally, the Bank, through its inclusive growth agenda, aims to support the reduction of women’s increased vulnerability and prevent mother-to-child HIV transmission. Addressing the gender dimension is an important priority in the response to the epidemic. Recent progress suggests that the solutions are in our hands. We can reduce gender inequalities by empowering women with information and services to prevent and treat HIV. Strategies to counter and manage gender-based violence can be effectively included in HIV-prevention programs. Effective treatment to reduce mother-to-child HIV transmission now needs to be scaled up and made accessible to those who need them, regardless of their socioeconomic status. Training health workers to provide gender-friendly counseling and services must also be prioritized. Most importantly, we need to sensitize men and elicit their involvement to create a supportive environment for reducing women’s vulnerabilities to the epidemic.

Getting to zero starts with us. It is time for Bank staff to take care of themselves and their families by taking advantage of HIV/AIDS services the Bank’s Medical Centre provides. These include Anonymous Voluntary Confidential Counseling and testing available to all Bank staff and their families.

I also want to stress that the African Development Bank is a workplace of zero discrimination and that we must support each other in our communities and workplace. Our fight to get to zero is producing results. Let’s continue in order to give the next generation of Africans – our children, our sons and daughters -- an AIDS-free life ahead. Zero has a value!

Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group

Distributed by APO (African Press Organization) on behalf of the African Development Bank (AfDB).

SOURCE 
African Development Bank (AfDB)

Tuhuma zang’oa maofisa Maliasili

Written By Unknown on Ijumaa, 29 Novemba 2013 | 13:30



Waziri wa Maliasili ya Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki akifungua mkutano wa wadau wa wanyamapori Dar es Salaam, jana. Picha na Emmanuel Herman 
Na Elizabeth Edward, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Novemba28  2013  saa 10:23 AM
Kwa ufupi
  • Akizungumza baada ya kufungua warsha ya wadau wa wanyamapori jana, Balozi Kagasheki alisema mapambano dhidi ya ujangili yanakabiliwa na changamoto nyingi kutokana na kuhusisha mtandao mkubwa ambao ndani yake kuna watu wazito na vigogo serikalini.
SHARE THIS STORY
0
Share


Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki amesema wizara yake imewasimamisha kazi baadhi ya maofisa kutokana na kujihusisha na biashara haramu ya ujangili wa meno ya tembo.
Akizungumza baada ya kufungua warsha ya wadau wa wanyamapori jana, Balozi Kagasheki alisema mapambano dhidi ya ujangili yanakabiliwa na changamoto nyingi kutokana na kuhusisha mtandao mkubwa ambao ndani yake kuna watu wazito na vigogo serikalini.
“Biashara hii wacha bwana, ni ngumu kwelikweli, inahusisha mtandao mkubwa… tayari tumewasimamisha baadhi ya watumishi na hivi karibuni nitayaweka wazi majina ya vigogo na watu wengine wanaojihusisha na mtandao huu.
“Haitaishia kuwasimamisha kazi tu, hatua zaidi dhidi yao zitachukuliwa kwani kujihusisha na vitendo vya ujangili ni sawa na kuhujumu uchumi wa Watanzania,” alisema Balozi Kagasheki.
Hata hivyo, Balozi Kagasheki amekuwa akitoa ahadi ya kuwataja vigogo wanaojihusisha na ujangili bila kutekeleza.
Kauli hiyo ya Kagasheki imekuja zikiwa zimepita wiki tatu tangu Rais Jakaya Kikwete kusitisha kwa muda Operesheni Tokomeza, lengo likiwa ni kutoa nafasi kwa Serikali kujipanga na kurekebisha kasoro zilizojitokeza kwenye awamu ya kwanza ya operesheni hiyo.
Balozi Kagasheki alisema rushwa na kukosekana kwa utashi wa kisiasa ndiyo sababu inayochangia kuwapo kwa changamoto kubwa katika vita dhidi ya biashara hiyo haramu, inayohatarisha maisha ya tembo na soko la utalii.
“Hii ni rasilimali ya Watanzania, hivyo hatutaweza kuvumilia watu wachache wanufaike,” alisema.

 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377