HABARI MPYA
blink

NAFASI ZA KAZI

Written By Unknown on Jumatatu, 6 Oktoba 2014 | 22:19


KAMA UNASAKA AJIRA ANGALIA HAPA
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/vacancies1.jpg

MASJALA YA ARDHI YACHOMWA KUFICHA UOVU

Written By Unknown on Ijumaa, 3 Oktoba 2014 | 08:28



Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma linawashikilia watu wanne kwa tuhuma za kuchoma moto Masijala ya Idara ya Ardhi ya Manispaa ya Kigoma Ujiji na kuteketeza Hati na Nyaraka mbali mbali za idara hiyo

Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma, ACP Jafari Mohamed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa wanaoshikiliwa watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Kamanda Mohamed amewataja watu hao kuwa ni Anna Fanuel (46), mhudumu wa ofisi, Makrina Paul (49),Karani, Saimon Pius (37),mkazi wa Burega na Tumaini Esau (44), mkazi wa Mwasenga, Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Alisema kuwa mnamo Octoba mosi mwaka huu majira ya saa nne na robo usiku Masijala ya Idara ya Ardhi ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ilichomwa moto na kuteketeza hati na nyaraka mbali mbali kitendo ambacho ni kinyume cha Sheria.

Inadaiwa kuwa kitendo hicho ni njama ya kupoteza vielelezo nyeti kutokana Idara hiyo kughubikwa na migogoro inayohusiana na ugawaji wa viwanja.

Kamanda Mohamed alisema mbinu iliyotumika ni kuchoma ofisi kwa kutumia mafuta ya Petroli.

MFUMO DUME WAKWAZA WANAWAKE TANZANIA

Written By Unknown on Alhamisi, 2 Oktoba 2014 | 09:07



Imeelezwa kuwa mfumo dume ni moja ya changamoto zinazokwamisha wananwake nchini Tanzania katika harakati za kushiriki uongozi wa kijamii na uchumi.

Hayo yamebainishwa na afisa kutoka shirika la umoja wa mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, Bi. Rose Mwalimu katika mahojiano maalumu.

Bi. Rose amebainisha kuwa wanawake wananyimwa fursa kutokana na mfumo dume jambo ambalo linatia shaka kama usawa wa hamsini kwa hamsini utapatikana ifikapo 2015 katika uwakilishi wa vyombo vya maamuzi.

Aidha Bi. Rose amebainisha kuwa licha ya jamii kutegemea vyombo vya habari katika kubadili tabia kwa njia ya habari, bado waandishi wa habari Tanzania havijatoa mchango wake kuondoa mfumo dume na unyanyasaji wa kijinsia

Akielezea juu ya weledi wa waandishi wa habari Tanzania Bi Rose mwalimu ambaye pia kitaaluma ni veteran katika taaluma ya habari, amewatahadharisha waandishi wa habari kuwa makini na waepuke kuandika habari zenye kuchochea migogoro.

Shirika la UNESCO linaendesha mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka katika Radio jamii nchini ili kuwajengea uwezo wa kuandika habari na kuandaa vipindi kwa kuzingatia masuala ya jinsi na jinsia.

Zaidi ya Radio Jamii 11 zimepata udhamini wa mafunzo na kujengewa uwezo na UNESCO ambayo yamefanyika kati ya September 22 na October mosi ambayo yamefanyika mkoani Kigoma pamoja na Mwanza.

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI

Written By Unknown on Jumatano, 17 Septemba 2014 | 07:13



MPANDA RADIO FM
Jengo la Kituo cha Matangazo cha Mpanda Radio FM 97.0 MHz mkoani Katavi

Iliyoko mjini Mpanda Mkoani Katavi, inatangaza nafasi za kazi kwa vijana wenye elimu, taaluma na kipaji cha uandishi wa habari na utangazaji. Muombaji anatakiwa awe na uzoefu wa angalau miaka miwili kazini.
Anayependa kufanya kazi Mpanda Radio atume maombi na wasifu wake akiambatanisha na nakala ya kazi (word and voice clips 2) alizofanya ndani ya mwezi mmoja uliopita.
Maombi yatumwe kwa emaili manager.mpandafm@gmail.com

WAHANGA WA MVUA 2013 WATELEKEZWA KIGOMA

Written By Unknown on Jumapili, 14 Septemba 2014 | 09:42

Na. Emanuel Senny, Kigoma. 
Bi. Bahati Luseba akiwa na wanawe katika eneo ilipokuwa nyumba yake


WAHANGA 100 wa mafuliko yaliyotokea mwaka 2013 maeneo ya katosho, kata ya Kibirizi katika manispaa ya Kigoma Ujiji wameachwa bila msaada wowote huku wakiishi maisha ya kutangatanga sambamba na kutotakiwa kujenga upya kutokana na eneo hilo kutengwa ili kupisha ujenzi wa bandari ya nchi kavu. 

Akifafanua hilo Mjane Bahati Luseba alisema yeye ni miongoni mwa wahanga ambapo alipoteza nyumba yake na anaoishi kwa kutangatanga kutafuta mahali pa kuishi hali inayowalazimu watoto wake watano wakiwemo wawili wa kike walale katika nyumba isiyosalama huku akisubiri fedha za fidia ambazo hajui atapewa lini. 

 Alisema aliishi hapo zaidi ya miaka 40 ndipo Desemba ,2013 walipokutwa na mafuriko, ambayo yalibomoa nyumba yake na kumlazimu alale nje zaidi ya miezi kumi akisubiri hatma ya malipo ya fidia kutoka serikalini ili aondokane na adha ya kutangatanga . 

Baada ya nyumba yangu kuharibika, mganga wa zahanati ya jibulenu alinipa chumba kwa muda katika zahanati yake , na kwasasa nimesaidiwa na mwalimu Gombea baada ya kutoka kutoka katika Zahanati kwani ni mahari pa wagonjwa tu alisema Luseba. 
Mabaki ya nyumba ziliezuliwa na Kimbunga wakati mvua kali
 Aliongeza kuwa taarifa zilizotoka Halmashauri kuwa kuna nyumba alitaftiwa kwaajiri ya makazi sio kweli pia mahema ambayo inasemekana walipewa baadhi ya wahanga hakuziona kwahiyo taarifa sio za kweli kwani yeye bado anatangatanga. 

Dkt. wa Zahanati ya Jibulenu Abu Rashid alikiri kumhifadhi katika chumba kimoja katika zahanati kutokana na mvua zilizokuwa zikiendelea. 

Nilishindwa kuendelea kumhuhifadhi kutokana na sheria,kanuni na taratibu za kikazi kuwa, zahanati si makazi rasmi kwa asiye mgonjwa aliongeza Rashidi. 

Aidha Kagu Jumanne ambaye ni mmoja wa wahanga wa mafuriko alisema kuwa baada ya tukio viongozi walienda eneo husika na kuahidi kutoa msaada kwa waathirika wote ila mpaka sasa hakuna walichopewa na wanaendelea kuhifadhiwa kwa majirani. 

Akijibia malamiko hayo Diwani wa kata husika Rashid Yunus ambaye pia ni Kaimu Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji alisema changamoto ya kushindwa kuwasaidia wahanga wa mafuriko inatokana na idadai kubwa ya walengwa na walitoa tulubai 52 kwa kaya 9 sambamba na kuyafungia mabati ili kuepusha lawama kwa umma kutokana na hali duni za wahanga hao. 

Hata hivyo Yunus alisema kuwa manispaa, ilitoa mabati chakavu 70, ili wapewe wananchi wenye maisha duni , lakini kutokana na ukubwa wa familia hizo wameamua kuyafungia katika ofisi ya serikali ya mtaa wa kahabwa katosho wakisubiri mchakato wa kufidiwa kwa wahanga hao ambao eneo lao limeteuliwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Bandari kavu.

WALIMU 50 WILAYANI MOSHI WAADHIBIWA

Written By Unknown on Alhamisi, 11 Septemba 2014 | 04:13



Na. Frida Peter
Moshi



Zaidi ya waalimu wakuu 50  katika shule za msingi katika halmashauri za wilaya ya moshi mkoani Kilimanjaro wamevuliwa madaraka na  wengine wakihamishwa kutokana na  sababu mbalimbali ikiwemo uwezo mdogo wa utawala.

Hayo yamebainishwa na afisa elimu ya msingi wa wilaya ya Moshi Bw. Simoni Sheshe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ya serikali kutoa adhabu wa walimu hao

Bw. Sheshe amebainisha kuwa uchunguzi uliofanywa na idara ya elimu umebaini kuwa walimu hao wamekuwa na desturi ya kujipatia kipato kinyume cha sheria kwa kutoza fedha za vyeti kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba

Sheshe amesema kuwa kufikia kwa hatua hiyo  kulitokana na malalamiko ya muda mrefu  ya wazazi na wananfunzi wa shule hizo  na kwamba tume ya utumishi ya walimu na idara ya elimu imekuwa ikitoa onyo mara kadhaa lakini walimu hao walikaidi.

Amesema waalimu wakuu hao walikuwa na tabia ya kuwatoza kiasi cha elfu kumi kila mzazi anaye fika shuleni hapo kwaajili ya kuchukua cheti cha darasa la saba jambo ambalo ni kinyume na utaratibu na kwamba cheti hicho hutolewa bure bila ya malipo yoyote.

Hata hivyo, licha ya adhabu hiyo kupongezwa na wazazi, mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Moshi Bw Moris Mokoi amesema kuvuliwa madaraka peke yake haitoshi na na ameagiza mkurugenzi wa halmashauri kuchukua hatua zaidi za kisheria dhidi ya waalimu watakao bainika kufanya hivyo.
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377