HABARI MPYA
blink

MADAI YA POSHO BUNGE LA KATIBA YAKONGA MWAMBA

Written By Unknown on Jumatatu, 24 Februari 2014 | 00:08


Habari kutoka ndani ya kamati iliyoundwa na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba, Pandu Ameir Kificho ili kufuatilia madai hayo, zimedai kuwa baada ya uchunguzi wa kina, wajumbe wa kamati hiyo hawakuona sababu ya kupendekeza posho hizo kupandishwa.
                              
Taarifa hizo zilidai kuwa wajumbe hao wamefikia uamuzi huo baada ya kupitia viwango vya posho vinavyolipwa na  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali na Mashirika ya Umma.

Pia kamati hiyo ilichambua viwango vya posho walivyolipwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na viwango vya posho ya kujikimu vya Sh80, 000 kwa siku wanavyolipwa watumishi wa Serikali.

 “Hili jambo linahitaji busara sana na kutazama mazingira ya nchi pia, kwa hiyo wajumbe wale baada ya kuoanisha viwango vya posho vya taasisi mbalimbali wameona Sh300,000 zinatosha,” alisema mmoja wa wajumbe ambaye hakutaka jina lake kutajwa.

Mjumbe mwingine, ambaye pia hakutaka kutajwa, alisema kuwa watakaa leo kukamilisha taarifa ya utafiti wao, kabla ya kuikabidhi kwa Mwenyekiti Kificho.

Alisema pamoja na umuhimu wa kazi za mbunge, lakini isingekuwa rahisi kuongeza posho katika mazingira ya sasa, ambapo wananchi wanalia hali ngumu ya maisha

Alisema pamoja na umuhimu wa kazi za mbunge, lakini isingekuwa rahisi kuongeza posho katika mazingira ya sasa, ambapo wananchi wanalia hali ngumu ya maisha.

Wajumbe hao walioteuliwa na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalumu, Pandu Ameir Kificho ni William Lukuvi, Mohamed Abood Mohamed, Freeman Mbowe,  Paul Kimiti, Jenister Mhagama na Asha Bakari.

Awali, taarifa kutoka ndani ya Bunge zilidokeza kuwa wajumbe hao walikuwa wakutane jana saa 9:00 alasiri ili kuandaa ripoti itakayopelekwa kwa Kificho ikiwa imebeba ushauri kuwa kiwango cha sasa cha posho kinatosha. 

Sh300,000 wanazolipwa wajumbe wa Bunge Maalamu la Katiba zinajumuisha Sh80,000 kwa siku ambayo ni posho ya kujikimu na Sh220,000 kwa siku kama posho maalumu ya kuhudhuria kikao.

Posho maalumu ya Sh220,000 inajumuisha posho ya dereva inayopaswa iwe kati ya Sh40,000 na Sh45,000 kwa siku, usafiri wa ndani (mafuta ama teksi), mawasiliano na matumizi mengine binafsi.

Chanzo: Mwananchi.

MATOKEO KIDATO NA NNE 2013 TANZANIA

Written By Unknown on Ijumaa, 21 Februari 2014 | 14:41




Baada ya kipindi cha ukimya, hofu na mashaka kwa wahitimu wa elimu ya sekondari kidato cha nne mwaka jana 2013, Hatimae kitendawili kimetegeliwa

katika mtandao huu unaweza kusoma matokeo yako au ya mwanao, au ndugu jamaa namarafiki

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2013

MAVAZI YA NUSU UCHI NA PICHA ZA NGONO MARUFUKU UGANDA

Written By Unknown on Jumatano, 19 Februari 2014 | 04:33



Rais Yoweri Museveni ametia saini mswada wa sheria kali dhidi ya picha za ngono ambao unapinga pia uvaaji wa mavazi yasiyo ya heshima

Sheria hiyo inatajwa kulenga kukomesha uvaaji wa nguo nusu uchi, kwa wavulana na wasichana nchini humo kama sehemu ya kuendelea utamaduni wa taifa hilo na wa kiafrika

Wanaotajwa kuguswa zaidi na sheria hiyo na ngono na mavazi ni wana mitindo, wanavuziki ambao wanatajwa kuwa vinara ya kutembea uchi hasa nyakati za maonesho ya kazi zao na wawapo katika hafla mbalimbali za kijamii

Nguo hasa yanayovaliwa na wanamziki na picha za watu wakiwa uchi. Mwandishi wetu wa Kampala Leylah Ndinda na taarifa zaidi. Kusikiliza taarifa hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Wakazi wan chi ya Uganda wanaopenda kuvaa nguo fupi, zinazobana au zinazoonyesha sehemu za mwili ambazo zaweza kuwafanya watu wa jinsia nyingine kusisimka na kutamani kushiriki ngono nawe, basi jua kuwa unachungulia jela.

RELIGIOUS SURPRISE STORY FOR AFRICA FROM EUROPE

Written By Unknown on Jumatatu, 17 Februari 2014 | 07:43



 

Prosper Kwigize, RNTC Hilversum, The Netherlands

My journey to Holland for study has been quit revealing and interesting.
Before I set out for the tour, I thought that at last I would have the opportunity of relating with the people that brought Christianity to my country.
This thinking was informed by my perception that these missionary priests  most of them are  Dutch and here I am in their country.

One week after landing the Dutch land, on the Sunday morning I went in the Bussum Street in order to search church for worship, after walking for about one and half kilometers I found one good building looking as church because of cross fixed at its roof. I was too sure I have found a place of worship.  

I decided to walk up to the building closely. Surprisingly the people I met coming out of the massive structure did not appear to me as worshippers.
While a man came with a dog in his hands, the other old woman that followed him was carrying domestic materials. This naturally fired my curiosity to know more about this building.   

I decided to ask about what time the mass is going to take off, the answer comes with question “which church, this is not church young man, this is an apartments where people lives, sorry for that

After the very short and clear answer from the people who I discover that is among of church building renters; I have shocked to see that while Africa we are making fundraising every day to contribute money for built new churches after old one being full, in Europe they are renting and changing usage of church to become an apartment
The Christian church in Africa

The history of Christianity in Africa began during the earthly ministry of Jesus Christ, two thousand years ago.
The New Testament of the Bible mentions several events in which Africans were witnesses to the life of Christ and the ministry of the apostles.

MSANII LULU AKIRI KUMUUA KANUMBA


Katika hali isiyotarajiwa na wengi, msanii maarufu Elizabeth maarufu LULU leo amekiri katika mahakama kuwa alimuua bila kukusudia msanii marufu Tanzania Steven Kanumba

Mbele ya Jaji Rose Temba, Lulu akiongozwa na wakili wake, amesema kulitokea ugonvi baina yao uliopelekea tafulani na kifo cha Kanumba

Lulu ameieleza mahakama kuwa, Kanumba licha ya kuwa bosi wake alikuwa pia mpenzi wake na kwamba ulipotokea ugomvi na lulu kumpiga na kitu kizito Kanumba, alitoa taarifa kwa shemeji yake (mdogo wa Kanumba) kabla ya kukamatwa na polisi

wakili upande wa serikali Monica Mbogo amesema mashahidi kadhaa wapo tayari kutoa ushahidi juu ya Lulu kumua Kanumba kwa makusudi

Lulu alifikishwa kwa mara ya kwanza mahamani April 11 mwaka 2012 ambapo alisomewa shitaka la mauaji na kulazimika kukaa rumande kwa miezi sita kabla ya kupata dhamana

NEC CCM YAMALIZIKA KWA AMANI


Licha ya watu wengi kuhofia kuwa, halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi iliyoketi jana mjini Dodoma kuwa kungekuwa na sintofahamu, wakubwa hao wamemaliza kikao chao kwa amani na mikakati ya maendeleo

Baadhi ya kurasa za mitandao ziliibuka na vichwa vya habari ambavyo vilihofisha kuwepo kwa mgawanyiko au kufukuzwa kwa baadhi ya wanachama, lakini jambo hilo halikuwepo

Kikao cha halmashauri kuu kilitanguliwa na vikao vingine vya uongozi wa chama kikiwemo cha maadili kilichowakutanisha wana CCM wanaotajwa kuwa na nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wengi wa wasomaji na wachangiaji katika mitandao walikuwa wakihofia kuwa huenda kukawa na kufukuzana ndani ya chama au baadhi yao kupigwa marufuku kugombea.

MBUNGE WA NZEGA -CCM ATOA TAMKO KUHUSU BUNGE LA KATIBA

Written By Unknown on Jumapili, 16 Februari 2014 | 14:26



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA



BUNGE LA TANZANIA

OFISI YA MBUNGE, JIMBO LA NZEGA

Mhe. Dkt. Hamisi A. Kigwangalla (MB),
Mwenyekiti, Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

KUMB. NA. MP/PR/001/2014                                                                       Tarehe: Feb 14, 2014

TAMKO LANGU KWA UMMA KUHUSU MCHAKATO WA KUANDIKA KATIBA MPYA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 

Ndugu wanahabari na waTanzania wenzangu,

Nimekuwa nikilazimika kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wanahabari, ndugu, jamaa na marafiki kuhusiana na namna mchakato wa kuandika katiba mpya ya Taifa letu unavyoenda; wengi wakipenda kujua nini mtazamo wangu kuhusu mambo mengi, haswa hili la serikali mbili ama tatu kwenye muungano wetu. Mara nyingi nimekuwa nikikwepa kusema msimamo wangu ni nini kwa sababu niliona ni vema nikajipa muda wa kutafakari kabla ya kuamua kujenga msimamo yangu. Ila kwa kuwa wakati wa kwenda Bungeni umefika na mimi nimepata bahati ya kuwa miongoni mwa wajumbe wa Bunge hili la kihistoria nimeona leo nitoe mtazamo wangu.

Kwanza, nianze kwa kuonesha wasiwasi wangu kama tutaweza kufika salama huko tuendako. Si kwa sababu za kitabiri kama mnajimu, la, ni kwa sababu za kisayansi, ambazo nitaziweka wazi hapa kama ifuatavyo:

(i.)                        Pamoja na kwamba tume imefanya kazi nzuri ya kukusanya maoni na kuyaweka katika nyaraka ambayo tutapaswa kuifanyia kazi, napata shida kama walikuwa makini katika kuendesha zoezi hili. Kivipi, binafsi napata shida na methodology iliyowawezesha kufikia ‘conclusion’ madhubuti kwamba watanzania asilimia 61 walitaka serikali tatu. Kwa sababu za kisayansi naona tume ya Mhe. Jaji Warioba imepotoka na kwamba kusema hivyo ni kutaka kulazimisha uhalali wa hoja hii nyeti kwenye dokumenti ya Rasimu ya Katiba tunayopaswa kuipitisha bila kuwa na msingi wa kitakwimu unaotokana na njia (methodology) za kisayansi za kukusanya ‘data’ na kutafuta ‘validity’ na ‘generalizability’ ya taarifa husika.  Nilidhani hili milikuwa na muda wa kutosha kama chama na kama wabunge kulitizama. Inasikitisha sana kusikia kuwa leo ndio linaonekana.

       

(ii.)                      Kwa jinsi mchakato ulivyo ni ngumu kusema kuwa leo tutaweza kubadili jambo nyeti kama la ‘Muundo wa Muungano’ kuwa uwe ni wa Serikali mbili, ama moja, wakati mapendekezo ya Tume, ambayo ‘yanaelezewa’ na Tume kuwa yanatokana na ‘maoni’ ya wananchi walio wengi, 61% na pili mabaraza ya katiba [cf. Muundo katika mchakato huu ni wa pyramid, kwamba unaanza na maoni ya wengi huku chini kwenye kitako, baadaye mabaraza ya katiba hapo katikati na mwisho Bunge la Katiba, kabla ya kura ya maoni]. Hivi inawezekana wapi Bunge Maalum la Katiba, kwa hapa tulipofikia, likafanya mabadiliko kwenye mambo yanayohusu ‘muundo’ (structure) wa Katiba? Yaani, kwamba inawezekana vipi wajumbe hawa 640 wabadilishe jambo zito la kimuundo kama hili? Kimantiki haingii akilini. Uhalali huo unatoka wapi? Lakini pia hapa hatuwezi kuondoa ukweli kwamba malalamiko na manung’uniko ya baadhi ya watu yana mashiko, kuwa hivi kama hoja ya Chama Cha Mapinduzi ilikuwa ni kuilinda ‘status quo’ ya muungano wa serikali mbili na kama walifanya kazi ya kuwaelimisha wanaCCM nchini, na wanaCCM walikuwa wengi zaidi kwenye mabaraza ya katiba ya wilaya [walishinda kwa zaidi ya asilimia 65, inatokeaje asilimia 61 watake muungano wa serikali 3?]. Maana yake ni kuwa hata wanachama wa ccm ngazi ya wilaya walichagua serikali tatu. Au inawezekana kuwa walitumwa kutoe hiyo elimu /maelekezo hawakuwa na nguvu (mbinu na weledi) ya ushawishi. Lakini pia ni somo kuwa sio sawa kuamini kuwa wanachama wa ccm ngazi ya wilaya hawawezi kutafakari na kuchagua, eti wao ni wa kupewa elimu na kufuata tu.  

 

Nini tafsiri ya haya yote? Kwamba ukisema unabadili leo muundo wa Muungano ukaleta wazo tofauti na lile linalotokana na mapendekezo ya tume, kama yanavyosomeka kwenye Rasimu (sura ya 6), mfano ukasema, ziwe serikali mbili tu badala ya tatu zinazopendekezwa, maana yake unaongelea kuanza upya kutengeneza vifungu vipya vya ‘kimuundo’ vya serikali za mitaa, wawakilishi wa wananchi, mambo ya wakuu wa mikoa ama majimbo(provinces) – jambo ambalo litakuwa cumbersome! Vurugu mechi bila uwepo wa rasimu! Swali la kujiuliza hapa ni kwamba – hivi tume hawakuliona hili? Pengine wangeweka chaguzi (option) pembeni, maana maoni yote haya wanayo, ila kwa sababu ya muundo wa Muungano ‘waliouchagua’ hawakupenda kuelezea mambo binafsi ya serikali hizi ‘mbili’ za ‘iliyokuwa Tanganyika’ na Zanzibar kwa madai kwamba jukumu lao ni kuandaa rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kinachoonekana hapa ni kwamba walikwishaamua kuwa ziwepo serikali tatu kwa madai kuwa ndiyo maoni ya wananchi na kwa kuzingatia msingi wa hoja kwamba Bunge la Katiba haliwezi kuwa na uhalali wa kubadili mambo ya msingi ya kimuundo wa katiba, kama hili la Muundo wa Muungano, bali ‘kuboresha’ tu yale yaliyomo. Mtu makini atahoji kuwa ni kwa nini wamekwepa kuzungumzia ukweli kwamba ‘Tanganyika’ hayupo? Na nini itakuwa hatma ya Katiba yake? Na ni lini wabia hawa wa Muungano walikaa wakakubaliana washirikiane kwenye mambo yapi kwenye huo muungano wa Shirikisho? Hili la tanzanyika kwa ujumla wake halikuwepo katika ToR na pia unajenga hoja kwa kuhisi tu hasa unaposema alikuwa “wameshaamua”.  

 

Sasa wabunge wa Bunge maalum la katiba tukiukataa huu muundo wa serikali tatu nini kitatokea? Maana yake sehemu kubwa ya rasimu hii italazimika kubadilishwa. Hakika ! Lakini kama ulivyosema wewe mwenyewe watapata wapi hayo mamlaka?

 

       Jambo lingine ambalo litatusumbua ni kuwa, vipi kama wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba tukiamua tujenge msimamo kwenye hoja ya Serikali Moja itakuwaje? Maswali mengi yataibuka bila kupata majibu hapa, kuwa ni nani atakuwa ‘Mpatanishi’ kwa niaba ya Tanganyika (ama Tanzania bara)? Maana Zanzibar yupo na ana uhai wake kamili, Tanganyika yuko wapi hapa? Hakika ! Lakini kama ulivyosema wewe mwenyewe watapata wapi hayo mamlaka? Na kama mkiamua hivyo mnatakiwa muwe na majibu ya hayo maswali na pia hamtahitaji siku 70 huko!

(iii.)              

 

Mhe. Jaji Joseph Warioba na wenzake wanapaswa wajibu maswali haya:

 

1.       Ni njia (methodology) ipi ya kisayansi na kitakwimu walitumia kufikia ‘conclusion’ hiyo madhubuti kabisa kuwa 61% ya watanzania walitaka Muundo wa Serikali Tatu? Watueleze watanzania sample size, sampling technique, sampling frame na namna walivyowafikia na kuwahoji watu hao. Hili jibu lake wanalo na hata wewe unajua watalijibu vizuri sana. Ingawa aliewapatia ToR anatakiwa kujua zaidi, vilevile ninashangaa ilikuwaje mkakubali rasimu ya kwanza bila kujua methodology nk ?

 

2.       Watueleze ni nani aliyewatuma kwenda kubadilisha Muundo wa Muungano?  Hapa nadhan kaka umesahau kuwa hawa jamaa walitumwa kukusanya maoni kuhusu Muungano, kimsingi unawezaje kuzungumzia muungano bila kuzungumzia muundo, na kama ukiuzungumzia, unawezaje kukwepa watu kuutolea maoni?

 

3.       Ni nani sasa atakuwa na mamlaka ya kuandika Katiba ya Serikali ya Tanganyika (ama Tanzania Bara – ambaye aliishakufa?), kama tukiamua kwenye Bunge la Katiba kupitisha Rasimu hii yenye Muundo wa Muungano wa Serikali tatu? Tunaanzia wapi kumfufua Tanganyika?

Hili ni swali zuri sana kaka, ila ninashangaa kwa nini wizara na mkuuw a nchi hajajibu mpaka sasa. Hili ni swali ambalo ninyi wabunge mlitakiwa kuliona kabla na kuhoji, ila kwa sababu mnazozijua ninyi hamkuhoji na leo unatoa tamko tu badala ya kuhoji wahusika…Kimsingi ukiwa mwenyekiti wa kamati ya TAMISEMI na ukijua kuwa ninyi ndio mhimili wa serikali na katiba ya Tanganyika na mpaka leo mnaona sawa tu kuendelea na mchakato bila majibu ya “iko wapi serikali ya mitaa na vijiji?” 

 

Maoni yangu: Mtu yeyote mpenda demokrasia ataona wazi kwamba kuna utata uliogubikwa na ukungu wa presha za kisiasa za kuona zoezi hili linakamilika. Utata wa uhalali wa Bunge la Katiba kubadili hoja za msingi kwenye rasimu ni jambo zito, na mashaka kwamba pengine Jaji Joseph Warioba na wenzake walikuwa na ajenda yao ya siku nyingi ya kuleta serikali tatu kinyume na matakwa ya Chama Tawala, CCM, ni jambo zito zaidi. Hivyo, kuondoa mamlaka na madaraka ya wananchi (kama kweli yapo kama inavyosema tume) kwenye jambo zito la kimsingi kama Muundo wa Muungano ni jambo linalotishia usalama wa mchakato na ni jambo lisilokubalika kwa kuwa linaondoa haki, wajibu, mamlaka na madaraka ya wananchi kufanya maamuzi kuhusu katiba yao (an act of popular sovereignity). Mkanganyiko huu unatia mashaka zaidi ya kuleta mwangaza wa mabadiliko ya kutokea kwa maridhiano. Jaji Warioba na wenzake walilijua hili na wameleta ‘chaos na frustration’ kwa maksudi kwa kujificha chini ya kivuli cha ‘uhalali’ wa Bunge la katiba HAO WENZAKE NI KINA NANI AMBAO HATA WAKO TAYARI KUWA KINYUME NA CCM ? HII INATISHA KIDOGO (yaani ‘legitimacy of rule or of law is based on the consent of the governed’) na nadharia pana ya demokrasia yenye msingi kwenye kanuni za ‘popular sovereignity’ wakijua kabisa wabunge tutashindana, tutatofautiana!

 

Mimi nina maoni kwamba, ili mchakato uishe salama, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete aingilie kati, atumie mamlaka yake kusitisha mchakato huu mpaka itakapoundwa tume nyingine ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu suala la Muundo wa Muungano na kisha ipigwe kura maalum ya maoni kuhusiana na jambo hili ili watanzania washiriki kikamilifu na waamue na siyo kufanya maamuzi ya kubadilisha Muundo wa Muungano bila kutupa fursa ya kujadiliana na kushiriki kufanya uamuzi kuhusu jambo hili. Ni jambo lisilo na busara hata kidogo kwenda kujadili Rasimu ya Katiba bila kuwa na suluhu inayokubalika kuhusu Muundo wa Muungano wetu. HAPA KAKA UMETUMIA MANENO MAKALI KIDOGO, YAANI HUONI BUSARA ? ANYWAY MIMI NINADHANI NDIO MAANA YA KWENDA KUJADILI UNLESS UNA WASIWASI NA UWEZO WA HAO WANAOTAKIWA KUJADILI…. ILA KAMA UNATAKA KUPATA “SULULU INAYOKUBALIKA” BILA KUJADILI SIDHANI KAMA UNAWEZA KUIPATA.   

 

Kama kuna presha ya muda wetu wa miaka mitano kuisha kuna dirisha la kutokea; tusogeze mbele muda wa uhai wa Uongozi wa awamu hii ama turudi nyuma tufanye mabadiliko ya sehemu za katiba zinazohusiana na Tume ya Uchaguzi tu. Hatuna namna ya kukwepa moja kati ya mambo haya kwa sababu hata tukifanikiwa kufunika kombe mwanaharamu apite, tukapitisha Katiba hii, INAONESHA KUWA HAKA KATABIA KAPO NA HUENDA KAMELETELEZA MKANGANYIKO AMBAO UNAUONA LEO, LAITI MSINGEKUWA MNAFUNIKA KOMBE LEO USINGEPATA SHIDA….bado tutahitaji kufanya mabadiliko makubwa ya Sheria mbalimbali nay a kitaasisi kutokana na Katiba mpya itakayokuwa imepatikana, zoezi ambalo kwa kila namna litahitaji muda wa kutosha na sioni kama upo! Demokrasia ni gharama na haikwepeki!

 

Maswali ni mengi zaidi ya Majibu. Wasiwasi ni mwingi kuliko uhakika. Tutafika salama kwenye kupata Katiba hii kweli? Ni bora tukawie kuliko kuvurunda. Tusikimbie kwa kasi bila kutazama tuendako, tutambae lakini macho njiani na mbele tunakoelekea.

 

Tamko hili limetolewa na Ofisi ya Mbunge, Jimbo la Nzega.

 

          HK (Nimesaini)

Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB.

NAFASI ZA MASOMO NA UDHAMINI WA ELIMU ULAYA


Kituo cha mafunzo ya uandishi wa habari na utangazaji wa kimataifa klichoko nchini Uholanzi knatangaza zaidi nafasi za masomo kwa waandishi wa habari wakongwe na chipukizi

kwa habari zaidi

course opportunity

MAKANISA ULAYA YAGEUZWA NYUMBA ZA KUPANGA

 
Ya Mungu mengi, wakati waafrika tukiamini kuwa wazungu wanampenda na kumthamini Mungu, na wakati wakristo waafrika wakithamini uwepo wa wazungu katika makanisa yao, Huku ulaya makanisa sasa yamefungwa na kugeuzwa kuwa nyumba za kuishi watu ...(nyumba za kupanga)
 
Baadhi ya Parokia na Parish sasa ni vituo vya kulelea watoto pamoja na maeneo ya biashara.
 
Leo nimetembelea katika Mji mmoja unaoitwa Bussum katikati ya nchi ya Holland nimeshangaa, kanisani nimekuta wazee na vikongwe tu tena hata robo ya kanisa hawajalijaza.
 
Udaku wangu haukuishia hapo nikaona ipo haja ya kujua kulikoni, ndipo nikaambiwa kuwa vijana na watu wenye umri wa kati aahhh makwao wakipumzika na kujiandaa na suluba za wili kuanzia kesho, jioni viwanja kula raha.......
 
Du ulikotoka umissionary ndiko kifo cha kanisa kinakoanzia. Jengo hilo la kanisa pichani sasa ni makazi ya watu si la ibada tena, nani aingie humo kusali?
 
 
Du kweli ulistaajabu ya musa utaona ya filauni, Kanisa zuri kama hili lingehamia Kasulu hata watoro wangerudi kupata neon
 
Yote haya nayashuhudiwa wakati Afrika tukihangaika kujenga makanisha baada ya yale ya awali kukosa nafasi, waumini tunaongezeka.
Mwenyezi Mungu aendelee kuleta neema na Baraka kwa waumini wake ili hatimaye amani na upendo, furaha na matumaini viendelee kuwepo miongoni mwa wannadamu
Mungu Ibariki nchi yetu Tanzania ambako bado tunakuthamini na kukuheshimu.
 
makala hii pia itakuijia kwa lugha ya kiingereza,

MAJINA YA WAJUMBE WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA

Written By Unknown on Jumamosi, 8 Februari 2014 | 09:01


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UTEUZI WA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA

UTANGULIZI
1. Uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba Unatawaliwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura, 83 (The Constitutional Review Act, Cap 83). Sheria hii inaweka mamlaka ya uteuzi, masharti, taratibu, vigezo na mambo mengine yote yanayopaswa kuzingatiwa katika uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba. Kwa mujibu wa Kifungu cha 22 (2A) na (2 vigezo hivi vinajumuisha umri, jinsia, uzoefu, sifa na mahali anapotoka mjumbe husika.

2. Sheria hii inatamka aina tatu za Wajumbe wa Bunge la Katiba kama ifuatavyo:-
(i) Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
(ii) Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar; na
(iii) Wajumbe 201 kwa mujibu wa Kifungu Na. 22(1c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inaonyesha makundi mbalimbali 10 yanayohusika.

3. Makundi hayo ni kama ifuatavyo:-

(i) Taasisi zisizokuwa za Kiserikali (20)
(ii) Taasisi za Kidini (20)
(iii) Vyama vyote vya Siasa vyenye Usajili wa Kudumu (42);
(iv) Taasisi za Elimu (20);
(v) Watu wenye Ulemavu (20);
(vi) Vyama vya Wafanyakazi (19);
(vii) Vyama vinavyowakilisha Wafugaji (10);
(viii) Vyama vinavyowakilisha wavuvi (10);
(ix) Vyama vya Wakulima (20); na
(x) Vikundi vya Watu wenye Malengo yanayofanana (20).

4. Mchakato wa uteuzi ulianza kwa kutoa Tangazo la Mwaliko katika Gazeti la Serikali, Tangazo la Serikali Na 443 la tarehe 13 Desemba, 2013. Tangazo hilo lilitolewa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ili kuyaalika makundi yaliyotajwa kisheria kuwasilisha mapendekezo ya majina kwa ajili ya uteuzi katika Bunge laMaalum la Katiba. Aidha, Tangazo hilo la mwaliko lilitangazwa pia katika magazeti mbalimbali yanayosomwa hapa nchini. Pamoja na mambo mengine Tangazo la Mwaliko lilitamka ukomo wa muda wa Taasisi na Makundi kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wajumbe kuwa ni tarehe 02/01/2014.
5. Mapendekezo hayo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar, mapendekezo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

6. Kufuatia mwaliko huo, taasisi 554 kutoka Tanzania Bara na 178 kutoka Zanzibar ziliwasilisha mapendekezo yao. Mapendekezo hayo yalijumuisha majina 2,762 kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar mapendekezo hayo yalihusisha watu 874. Hivyo basi, taasisi na makundi mbalimbali yalipendekeza jumla ya majina 3,636. Lakini, na kinyume na Sheria, watu 118 walijipendekeza wenyewe na kufanya idadi ya majina yaliyopendekezwa kuwa 3,754.

7. Mchanganuo wa idadi ya watu walipendekezwa katika makundi mbalimbali ni kama ifuatavyo:

[TH]Na.[/TH][TH]Kundi/Taasisi[/TH][TH="colspan: 2"]Taasisi zilizoleta mapendekezo[/TH][TH="colspan: 2"]Idadi ya Watu Waliopendekezwa[/TH][TH]Idadi ya Wajumbe Wanaotakiwa[/TH][TH="colspan: 2"]Idadi ya Walioteuliwa[/TH]
[TH]Tanzania Bara[/TH][TH]Zanzibar[/TH][TH]Tanzania Bara[/TH][TH]Zanzibar[/TH][TH]Tanzania Bara[/TH][TH]Zanzibar[/TH]
1. Taasisi zisizokuwa za Kiserikali 246 98 1,203 444 20 13 7
2. Taasisi za Kidini 55 17 344 85 20 13 7
3. Vyama vya Siasa vyenye Usajili wa Kudumu 21 14 129 69 42 28 14
4. Taasisi za Elimu 9 9 84 46 20 13 7
5. Makundi ya Walemavu 24 6 97 43 20 13 7
6. Vyama vya Wafanyakazi 20 1 89 13 19 13 6
7. Vyama Vinavyowakilisha Wafugaji 8 1 43 4 10 7 3
8. Vyama vinavyowakilisha Wavuvi 7 3 45 12 10 7 3
9. Vyama vya Wakulima 22 8 115 44 20 13 7
10. Makundi yenye Malengo Yanayofanana 142 21 613 114 20 14 6
Mapendekezo Binafsi - - 118 -
Jumla 672 178 2,880 874 201 134 67
Jumla Kuu 850 3,754

8. Sheria ya Mabadiliko ya Katiba imeweka masharti ya kuzingatiwa katika uteuzi wa wajumbe 201 wa Bunge la Maalum la Katiba. Masharti hayo ni pamoja na wajumbe wasiopungua theluthi moja wanatakiwa kutoka Zanzibar na theluthi mbili kutoka Tanzania Bara. Kwa sababu hiyo, katika wajumbe 201, wajumbe 67 watatoka Zanzibar na wajumbe 134 watatoka Tanzania Bara. Aidha, mgawanyo wa wajumbe wanawake na wanaume unatakiwa uwe nusu kwa nusu. Pamoja na hayo, wajumbe hao wawakilishe sura ya wananchi wa Tanzania kwa ufuasi wa vyama vya siasa, dini, umri, na maeneo wanayotoka. Katika mazingira haya, zoezi la kupata wajumbe 201 halikuwa rahisi hata kidogo. Mwitikio wa makundi ulikuwa mkubwa sana ikilinganishwa na nafasi zilizopo.
9. Kama nilivyoeleza hapo awali, mapendekezo kutoka Tanzania Bara yalikuwa 2,880 wakati nafasi za wajumbe ni 134. Kwa upande wa Zanzibar, majina yaliyopendekezwa yalikuwa 874 ikilinganishwa na idadi ya wajumbe 67 wanaotakiwa kuteuliwa. Kwa nyongeza ya maelezo kuhusu uwingi wa mapendekezo, ni kwamba ukichukua taasisi zisizo za kiserikali kwa upande wa Tanzania Bara walipendekezwa watu 1,203, wakati nafasi zilizokuwa zinatakiwa kujazwa ni 13 tu. Kwa upande Zanzibar, taasisi zisizokuwa za kiserikali zilikuwa zimependekeza majina 444 ikilinganishwa na nafasi 7 tu zilizokuwa zinatakiwa kujazwa kutokana na taasisi hizi.

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA
10. Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania wakishirikiana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mpainduzi Zanzibar wamekamilisha uteuzi wa wajumbe 201. Kabla ya kutaja orodha ya wajumbe walioteuliwa, napenda kufafanua mambo yafuatayo:
(a) Uteuzi umezingatia ushiriki wa watu wa rika zote, yaani vijana, watu wazima na wazee. Kwa ajili hiyo, wajumbe vijana yaani wenye umri wa kati miaka 22-35, ni wajumbe 35. Wajumbe wenye umri wa kati, yaani miaka 36-64, ni 145; na wajumbe wazee, yaani wenye umri wa miaka 65 na kuendelea ni 21.
(b) Sheria inataka kuwepo na uwiano sawa kwa ajumbe wanawake na wanaume. Jambo hili limezingatiwa ipasavyo, na katika orodha hii wajumbe wanawake ni 100 na wanaume 101. Kwa vile, haiwezekani kuwa na nusu mtu, ndiyo maana idadi ya wajumbe wanaume ni 101.
(c) Uwakilishi wa vyama vya siasa ambao unahitaji kila chama chenye usajili wa kudumu kiwe na wajumbe wawili umezingatiwa. Kwa kuwa kuna vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu 21, jumla ya wajumbe 42 wamechaguliwa kwa maana ya kuwa wajumbe wawili wameteuliwa kutoka katika kila chama.
Baada ya maelezo hayo ya utangulizi, ifuatayo ndiyo orodha ya wajumbe 201 wa Bunge Maalum la Katiba waliobahatika kuteuliwa:

TAASISI ZISIZOKUWA ZA KISERIKALI- (WAJUMBE 20)

TANZANIA BARA (13)

1. Magdalena Rwebangira 2. Kingunge Ngombale Mwiru
3. Asha D. Mtwangi 4. Maria Sarungi Tsehai
5. Paul Kimiti 6. Valerie N. Msoka
7. Fortunate Moses Kabeja 8. Sixtus Raphael Mapunda
9. Elizabeth Maro Minde 10. Happiness Samson Sengi
11. Evod Herman Mmanda 12. Godfrey Simbeye
13. Mary Paul Daffa
TANZANIA ZANZIBAR (7)
1. Idrissa Kitwana Mustafa 2. Siti Abbas Ali
3. Abdalla Abass Omar 4. Salama Aboud Talib
5. Juma Bakari Alawi 6. Salma Hamoud Said
7. Adila Hilali Vuai

TAASISI ZA KIDINI- (WAJUMBE 20)
TANZANIA BARA (13)
1. Tamrina Manzi 2. Olive Damian Luwena
3. Shamim Khan 4. Mchg. Ernest Kadiva
5. Sheikh Hamid Masoud Jongo 6. Askofu Mkuu (Mstaafu) Donald Leo Mtetemela
7. Magdalena Songora 8. Hamisi Ally Togwa
9. Askofu Amos J. Muhagachi 10. Easter Msambazi
11. Mussa Yusuf Kundecha 12. Respa Adam Miguma
13. Prof. Costa Ricky Mahalu
TANZANIA ZANZIBAR (7)
1. Sheikh Thabit Nouman Jongo 2. Suzana Peter Kunambi
3. Sheikh Nassoro Mohammed Ibrahimu 4. Fatma Mohammed Hassan
5. Louis Majaliwa 6. Yasmin Yusufali E. H alloo
7. Thuwein Issa Thuwein

VYAMA VYOTE VYA SIASAVYENYE USAJILI WA KUDUMU – (WAJUMBE 42)
TANZANIA BARA (2
1. Hashim Rungwe Spunda 2. Thomas Magnus Mgoli
3. Rashid Hashim Mtuta 4. Shamsa Mwangunga
5. Yusuf S. Manyanga 6. Christopher Mtikila
7. Bertha Ng’angompata 8. Suzan Marwa
9. Dominick Abraham Lyamchai 10. Mbwana Salum Kibanda
11. Peter Kuga Mziray 12. Isaac Manjoba Cheyo
13. Dr. Emmanuel John Makaidi 14. Prof. Ibrahim Haruna Lipumba
15. Modesta Kizito Ponera 16. Prof. Abdallah Safari
17. Salumu Seleman Ally 18. James Kabalo Mapalala
19. Mary Oswald Mpangala 20. Mwaka Lameck Mgimwa
21. Nancy S. Mrikaria 22. Nakazael Lukio Tenga
23. Fahmi Nasoro Dovutwa 24. Costantine Benjamini Akitanda
25. Mary Moses Daudi 26. Magdalena Likwina
27. John Dustan Lifa Chipaka 28. Rashid Mohamed Ligania Rai
TANZANIA ZANZIBAR (14)
1. Ally Omar Juma 2. Vuai Ali Vuai
3. Mwanaidi Othman Twahir 4. Jamila Abeid Saleh
5. Mwanamrisho Juma Ahmed 6. Juma Hamis Faki
7. Tatu Mabrouk Haji 8. Fat –Hiya Zahran Salum
9. Hussein Juma 10. Zeudi Mvano Abdullahi
11. Juma Ally Khatibu 12. Haji Ambar Khamis
13. Khadija Abdallah Ahmed 14. Rashid Yussuf Mchenga

TAASISI ZA ELIMU- (WAJUMBE 20)
TANZANIA BARA
1. Dr. Suzan Kolimba 2. Prof. Esther Daniel Mwaikambo
3. Dr. Natujwa Mvungi 4. Prof. Romuald Haule
5. Dr. Domitila A.R. Bashemera 6. Dr. Jasmine Bendantunguka Tiisekwa
7. Prof. Bernadeta Kilian 8. Teddy Ladislaus Patrick
9. Dr. Francis Michael 10. Prof. Remmy J. Assey
11. Dr. Tulia Ackson 12. Dr. Ave Maria Emilius Semakafu
13. Hamza Mustafa Njozi
TANZANIA ZANZIBAR (7)
1. Makame Omar Makame 2. Fatma Hamid Saleh
3. Dr. Aley Soud Nassor 4. Layla Ali Salum
5. Dkt. Mwinyi Talib Haji 6. Zeyana Mohamed Haji
7. Ali Ahmed Uki

WATU WENYE ULEMAVU-(WAJUMBE 20)
TANZANIA BARA (13)
1. Zuhura Musa Lusonge 2. Frederick Msigala
3. Amon Anastaz Mpanju 4. Bure Zahran
5. Edith Aron Dosha 6. Vincent Venance Mzena
7. Shida Salum Mohamed 8. Dr. Henry Mwizengwa Nyamubi.
9. Elias Msiba Masamaki 10. Faustina Jonathan Urassa
11. Doroth Stephano Malelela 12. John Josephat Ndumbaro
13. Ernest Njama Kimaya
TANZANIA ZANZIBAR (7)
1. Haidar Hashim Madeweyya 2. Alli Omar Makame
3. Adil Mohammed Ali 4. Mwandawa Khamis Mohammed
5. Salim Abdalla Salim 6. Salma Haji Saadat
7. Mwantatu Mbarak Khamis
VYAMA VYA WAFANYAKAZI-(WAJUMBE 19)
TANZANIA BARA (13)
1. Honorata Chitanda 2. Dr. Angelika Semike
3. Ezekiah Tom Oluoch 4. Adelgunda Michael Mgaya
5. Dotto M. Biteko 6. Mary Gaspar Makondo
7. Halfani Shabani Muhogo 8. Yusufu Omari Singo
9. Joyce Mwasha 10. Amina Mweta
11. Mbaraka Hussein Igangula 12. Aina Shadrack Massawe
13. Lucas Charles Malunde
TANZANIA ZANZIBAR (6)
1. Khamis Mwinyi Mohamed 2. Jina Hassan Silima
3. Makame Launi Makame 4. Asmahany Juma Ali
5. Mwatoum Khamis Othman 6. Rihi Haji Ali

VYAMA VINAVYOWAKILISHAWAFUGAJI-(WAJUMBE 10)
TANZANIA BARA (7)
1. William Tate Olenasha 2. Makeresia Pawa
3. Mabagda Gesura Mwataghu 4. Doreen Maro
5. Magret Nyaga 6. Hamis Mnondwa
7. Ester Milimba Juma
TANZANIA ZANZIBAR (3)
1. Said Abdalla Bakari 2. Mashavu Yahya
3. Zubeir Sufiani Mkanga

VYAMA VINAVYOWAKILISHAWAVUVI –(WAJUMBE 10)
TANZANIA BARA (7)
1. Hawa A. Mchafu 2. Rebecca Masato
3. Thomas Juma Minyaro 4. Timtoza Bagambise
5. Tedy Malulu 6. Rebecca Bugingo
7. Omary S. Husseni
TANZANIA ZANZIBAR (3)
1. Waziri Rajab 2. Issa Ameir Suleiman
3. Mohamed Abdallah Ahmed

VYAMA VYAWAKULIMA-(WAJUMBE 20)
TANZANIA BARA (13)
1. Agatha Harun Senyagwa 2. Veronica Sophu
3. Shaban Suleman Muyombo 4. Catherine Gabriel Sisuti
5. Hamisi Hassani Dambaya 6. Suzy Samson Laizer
7. Dr. Maselle Zingura Maziku 8. Abdallah Mashausi
9. Hadijah Milawo Kondo 10. Rehema Madusa
11. Reuben R. Matango 12. Happy Suma
13. Zainab Bakari Dihenga
TANZANIA ZANZIBAR (7)
1. Saleh Moh’d Saleh 2. Biubwa Yahya Othman
3. Khamis Mohammed Salum 4. Khadija Nassor Abdi
5. Fatma Haji Khamis 6. Asha Makungu Othman
7. Asya Filfil Thani

WATU WENYE MALENGO YANAYOFANANA – (WAJUMBE 20)
TANZANIA BARA (14)
1. Dr. Christina Mnzava 2. Paulo Christian Makonda
3. Jesca Msambatavangu 4. Julius Mtatiro
5. Katherin Saruni 6. Abdallah Majura Bulembo
7. Hemedi Abdallah Panzi 8. Dr. Zainab Amir Gama
9. Hassan Mohamed Wakasuvi 10. Paulynus Raymond Mtendah
11. Almasi Athuman Maige 12. Pamela Simon Massay
13. Kajubi Diocres Mukajangwa 14. Kadari Singo
TANZANIA ZANZIBAR (6)
1. Yussuf Omar Chunda 2. Fatma Mussa Juma
3. Prof. Abdul Sheriff 4. Amina Abdulkadir Ali
5. Shaka Hamdu Shaka 6. Rehema Said Shamte

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
7 Februari, 2014
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377