HABARI MPYA
blink
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo News. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo News. Onyesha machapisho yote
07:13
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI
Written By Unknown on Jumatano, 17 Septemba 2014 | 07:13
MPANDA RADIO
FM
| Jengo la Kituo cha Matangazo cha Mpanda Radio FM 97.0 MHz mkoani Katavi |
Iliyoko mjini Mpanda Mkoani Katavi,
inatangaza nafasi za kazi kwa vijana wenye elimu, taaluma na kipaji cha
uandishi wa habari na utangazaji. Muombaji anatakiwa awe na uzoefu wa angalau
miaka miwili kazini.
Anayependa kufanya kazi Mpanda Radio
atume maombi na wasifu wake akiambatanisha na nakala ya kazi (word and voice
clips 2) alizofanya ndani ya mwezi mmoja uliopita.
Maombi yatumwe kwa emaili
manager.mpandafm@gmail.com
04:13

Na. Frida Peter
Moshi
Hata hivyo, licha ya
adhabu hiyo kupongezwa na wazazi, mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Moshi Bw
Moris Mokoi amesema kuvuliwa madaraka peke yake haitoshi na na ameagiza
mkurugenzi wa halmashauri kuchukua hatua zaidi za kisheria dhidi ya waalimu
watakao bainika kufanya hivyo.
WALIMU 50 WILAYANI MOSHI WAADHIBIWA
Written By Unknown on Alhamisi, 11 Septemba 2014 | 04:13

Na. Frida Peter
Moshi
Zaidi ya waalimu wakuu 50 katika shule za
msingi katika halmashauri za wilaya ya moshi mkoani Kilimanjaro wamevuliwa
madaraka na wengine wakihamishwa kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo uwezo mdogo wa utawala.
Hayo yamebainishwa na afisa elimu ya msingi wa wilaya ya Moshi
Bw. Simoni Sheshe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ya
serikali kutoa adhabu wa walimu hao
Bw. Sheshe amebainisha kuwa uchunguzi uliofanywa na idara ya
elimu umebaini kuwa walimu hao wamekuwa na desturi ya kujipatia kipato kinyume
cha sheria kwa kutoza fedha za vyeti kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba
Sheshe amesema kuwa kufikia kwa hatua hiyo kulitokana
na malalamiko ya muda mrefu ya wazazi na wananfunzi wa shule hizo na
kwamba tume ya utumishi ya walimu na idara ya elimu imekuwa ikitoa onyo mara
kadhaa lakini walimu hao walikaidi.
Amesema waalimu wakuu hao walikuwa na tabia ya kuwatoza
kiasi cha elfu kumi kila mzazi anaye fika shuleni hapo kwaajili ya kuchukua
cheti cha darasa la saba jambo ambalo ni kinyume na utaratibu na kwamba cheti
hicho hutolewa bure bila ya malipo yoyote.
Labels:
News
10:16
MWANAFUNZI ABAKWA KIGOMA
Written By Unknown on Jumatano, 10 Septemba 2014 | 10:16
Na Emanuel Michael, Kigoma.
MWANAFUNZI wa darasa la saba miaka 14 amebakwa mapema wiki
hii kabla ya kuanza mtihani wa kumaliza elimu ya msingi katika kijiji cha
Bukuba, Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma.
Akizungumza na waandishi wa habari, Bi. Anisia Enock ambaye
ni mama wa mtoto huyo, alisema kuwa mtoto wake alibakwa na Amoni Samwel (25) mkazi
wa Mwanga B na kuhatarishiwa hatimayake ya kufanya mtihani.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 12 jioni wakati
mwanye huyo alipokuwa akielekea dukani kuchukua simu, mbani ndipo wazazi
walipohoji uchelewaji huo na mwanaye akaeleza alichotendewa na Amoni Samwel.
“Binti yangu aliponisimulia nilichanganyikiwa kwani
anatarajiwa kufanya mtihani Jumatano na nilipomchunguza
alikuwa akitokwa na damu zilizotapakaa
kwenye makalio ndipo nikaamua kumpigia simu baba yake kabla ya kwenda kwenye vyombo vya sheria”
alisema Bi. Enock.
Aidha Enock alisema kuwa alienda kutoa taarifa polisi na
baada ya kuandika mashtaka alipewa PF3 kwaajiri ya kwenda Hospitali na walipofika binti yake akafanyiwa
vipimo sambamba na kupatiwa matibabu.
“Siku ya jumatatu Maafisa usitawi wa Jamii walifika na
kumfanyia vipimo upya na kumpatia dawa tena ili kumpa nguvu ya kufanya mtihani”
aliongeza
Kwa upande wa mwanafunzi aliyebakwa jina linahifadhiwa, alisema kuwa baada ya kutumwa na mama yake
alikutana na mwanafunzi mwenzake wa kiume na kumuomba amuelekeze
walichofundishwa darasani na ndipo Amoni Samweli alipowakuta.
Aliongeza kuwa baada Mbakaji kuja aliwauliza walichokuwa
wanafanya, nao wakamjibu kuwa wanasoma
lakini yeye akakataa na kuanza kumpiga makofi yule mvulana sanjari na kumwambia
aondoke eneo mlile.
“Baada ya kumfukuza mwanafunzi mwenzangu alinambia nivue
nguo mimi nikakataa ndipo akanibeba na kunipeleka kwenye shamba la ndizi na kunifumba
mdomo ili nisipige kelele huku akinitishia kunichoma kisu hapo ndipo akanibaka”
aliongeza.
Nae Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Buhigwe, Godfrey
Kapaya alisema kuwa walifika nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kumfanyia vipimo
vilivyothibitisha tukio hilo na alikuwa na maumivu sehemu za siri.
“Baada ya hapo tulimpa dawa za maumivu, dawa za kuzuia
maambukizi ya magonjwa ya zinaa pamoja na mimba” alisema Kapaya.
Kapaya aliongeza kuwa kwakuwa mwanafunzi alitakiwa kuingia
kwenye mtihani walimpa ushauri wa kumuondolea
hofu ili afanye mtihani akiwa katika
hari nzuri ya kimawazo.
Pamoja na hayo Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma, Japhari
Muhamed alithibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa mtuhumiwa tayari yuko
mahabusu na hatua za kumfikisha mahakamani zinaendelea.
“Kitendo hiki ni kibaya sana na sisi tunakilaani kwani ndio
tunaolinda watoto na wananchi kwa ujumla sasa ili iwe fundisho kwa wengine
lazima mtuhumiwa ahukumiwe” alisema Muhamed.
Muhamed aliwataka wananchi kuwawaelimishe watoto wao
wasitembee sehemu zisizo salama wakiwa peke yao hasa mida ya usiku pia na
wazazi wawe makini kuwaacha watoto zao peke yao sambamba na kutoa taarifa pindi
wanaposikia matukio kama haya.
Mwisho.
Labels:
News
11:43
Mbunge Felix Mkosamali wa Jimbo la Muhambwe Nccr mageuzi amenusurika kifo baada ya gari alimokuwa akisafiria kutoka Dodoma kwenda Kigoma kupata ajali
Kwa mujibu wa Polisi mkoani Dodoma Mkosamali amepata ajali katika wilaya ya Bahi baada ya gari lake kuligonga kwa nyuma roli lililokuwa limeegesha pembeni ya barabara
Kwa mujubu wa taarifa hizo, watu watatu waliokuwemo ndani ya gari la Mbunge huyo wamejeruhiwa
inaelezwa kuwa chanzi cha ajali hiyo ni uzembe wa dreva wa gari la Mbunge huyo ambaye alishindwa kufuata alama za barabarani na kuwa katika mwenzo mkali uliosababisha ashindwe kulimudu gari hilo.
MBUNGE WA MUHAMBWE KIBONDO ANUSURIKA KIFO
Written By Unknown on Ijumaa, 5 Septemba 2014 | 11:43
![]() |
| Mhe. Felix Mkosamali Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Kibondo |
Kwa mujibu wa Polisi mkoani Dodoma Mkosamali amepata ajali katika wilaya ya Bahi baada ya gari lake kuligonga kwa nyuma roli lililokuwa limeegesha pembeni ya barabara
Kwa mujubu wa taarifa hizo, watu watatu waliokuwemo ndani ya gari la Mbunge huyo wamejeruhiwa
inaelezwa kuwa chanzi cha ajali hiyo ni uzembe wa dreva wa gari la Mbunge huyo ambaye alishindwa kufuata alama za barabarani na kuwa katika mwenzo mkali uliosababisha ashindwe kulimudu gari hilo.
Labels:
News
07:09
Habari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa watu wanane wamepoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea mchana mkoani Katavi
ajali hiyo imehusisha Roli la mizigo ambao watu kadhaa walipanda wakitokea wilaya ya Mlele kwenda mjini Sumbawanga
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa ajalii hiyo na kwamba imetokea katika mlima Katete ambapo lilishindwa kupanda na kupinduka.
Hadi tunaingia mitamboni askari wa usalama walikuwa eneo la tukio wakijaribu kuokoa majeruhi.
8 WAPOTEZA MAISA AJALINI KATAVI
Habari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa watu wanane wamepoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea mchana mkoani Katavi
ajali hiyo imehusisha Roli la mizigo ambao watu kadhaa walipanda wakitokea wilaya ya Mlele kwenda mjini Sumbawanga
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa ajalii hiyo na kwamba imetokea katika mlima Katete ambapo lilishindwa kupanda na kupinduka.
Hadi tunaingia mitamboni askari wa usalama walikuwa eneo la tukio wakijaribu kuokoa majeruhi.
Labels:
News
06:55
36 WAPOTEZA MAISHA BUTIAMA
Watu 36 wamefariki dunia
katika ajali ya magari mawili ya abiria wilayani Butiama mkoani mara mapema leo
Habari kutoka kwa jeshi la
polisi mkoani Mara zinasema kuwa ajali
hiyo imehusisha mabasi ya kampuni ya Mwanza Coach na J4 yanayofanya safari
kutoka Butiama kwenda Mwanza
Imeelezwa kuwa ajali hiyo
imetokea leo asubuhi katika eneo la sabasaba ambapo watu wengine 79
wamejeruhiwa na wanapatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya Butiama
Jeshi la polisi linafanya
uchunguzi zaidi kuhusu chanzo cha ajali hiyo
Labels:
News
03:59
BREAKING NEWS- HOFU YATANDA MJINI KASULU, BODABODA WAANDAMANA
Written By Unknown on Alhamisi, 4 Septemba 2014 | 03:59
Hofu imetanda
katika mji wa Kasulu kufuatia vurugu zinazofanywa na madreva pikipiki maarufu
kama Bodaboda ambao wanafanya maandamano kuelekea kituo cha polisi kushinikiza
wenzao wanaoshikiliwa waachiwe huru.
Hali hiyo
imeanza majira ya saa sita mchana baada ya kile wanachodai kuwa askari wa
usalama barabarani tangu asubuhi wamekuwa wakikamata bodaboda na kasha kuwapiga
bila makosa.
Barabara kuu
ya mjini Kasulu itokayo maeneo ya makaburini hadi kituo cha polisi imefurika
pikipiki zinazoendeshwa kwa fujo kuelekea mtaa wa mlimani kwa ajili ya
kushinikiza polisi kuwaachia wenzao waliokamatwa
Hata hivyo
habari zinaeleza kuwa, mtu mmoja leo amegongwa nagari eneo la soko kuu kutokana
na kile kinachoelezwa kuwa ni msongamano wa pikipiki zinazopaki katika makutano
ya barabara hali inayosababisha upishanaji wa watembea kwa miguu, magari na
pikipiki kuwa wa shida.
Mzee huyo
ambaye jina lake hadi sasa halijajulikana amelazwa katika hospitali ya wilaya
ya Kasulu.
Labels:
News
07:36
POLISI WAUA MAJAMBAZI WATANO KIGOMA
Written By Unknown on Jumatano, 3 Septemba 2014 | 07:36
Watu watano majambazi wanaodhaniwa
kuwa Raia wa Burundi wameuawawa katika majibizano ya risasi na askari Polisi
wilayani Kasulu
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma ACP Jafary Muhamed amesema
kuwa tukio hilo limetokea leo asubuhi katika eneo la Maragalasi na kwamba
walikuwa katika jaribio la kuteka mabasi yanayofanya safari zake kati ya
Kigoma, Dar es Salaam, Kahama na Mwanza.
Watatu kati ya waliouwawa walikuwa wamevaa sare za kijeshi
ambazo zinadhaniwa kuwa ni sare za jeshi la Burundi.
katika tukio hilo, Bunduki mbili
aina ya SMG, risasi 65za SMG na mabomu matatu ya kutupwa kwa mkono yamekamatwa
Polisi
wanaendelea na msako katika porii la Maragalasi ili kubaini kama kuwa kambi
inayotumika kuhifadhi silaha
Vijiji vinavyopakana
na pori la Maragalasi hususani Mvugwe na Busunzu vimekuwa vikikubwa na matukio
mengi ya uvamizi na uporaji unaohusisha silaha za kivita
Inaelezwa kuwa
matukio hayo yanawahusisha watanzania wanaoshirikiana na Raia wa Burundi
Mwezi uliopita
watu watano abiria waliokuwa wakisafiri kutoka vijiji vya mpakani mwa Tanzania na
Burundi walipoteza maisha baada ya gari lao kutekwa na kasha kutupiwa bomu la
kutupwa kwa mkono
Labels:
News






