Home » » POLISI WAUA MAJAMBAZI WATANO KIGOMA

POLISI WAUA MAJAMBAZI WATANO KIGOMA

Written By Unknown on Jumatano, 3 Septemba 2014 | 07:36



Watu watano majambazi wanaodhaniwa kuwa Raia wa Burundi wameuawawa katika majibizano ya risasi na askari Polisi wilayani Kasulu

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma ACP Jafary Muhamed amesema kuwa tukio hilo limetokea leo asubuhi katika eneo la Maragalasi na kwamba walikuwa katika jaribio la kuteka mabasi yanayofanya safari zake kati ya Kigoma, Dar es Salaam, Kahama na Mwanza.
Watatu kati ya waliouwawa walikuwa wamevaa sare za kijeshi ambazo zinadhaniwa kuwa ni sare za jeshi la Burundi.
katika tukio hilo, Bunduki mbili aina ya SMG, risasi 65za SMG na mabomu matatu ya kutupwa kwa mkono yamekamatwa

Polisi wanaendelea na msako katika porii la Maragalasi ili kubaini kama kuwa kambi inayotumika kuhifadhi silaha
Vijiji vinavyopakana na pori la Maragalasi hususani Mvugwe na Busunzu vimekuwa vikikubwa na matukio mengi ya uvamizi na uporaji unaohusisha silaha za kivita
Inaelezwa kuwa matukio hayo yanawahusisha watanzania wanaoshirikiana na Raia wa Burundi
Mwezi uliopita watu watano abiria waliokuwa wakisafiri kutoka vijiji vya mpakani mwa Tanzania na Burundi walipoteza maisha baada ya gari lao kutekwa na kasha kutupiwa bomu la kutupwa kwa mkono
Share this article :
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377