Home » » BREAKING NEWS- HOFU YATANDA MJINI KASULU, BODABODA WAANDAMANA

BREAKING NEWS- HOFU YATANDA MJINI KASULU, BODABODA WAANDAMANA

Written By Unknown on Alhamisi, 4 Septemba 2014 | 03:59



Hofu imetanda katika mji wa Kasulu kufuatia vurugu zinazofanywa na madreva pikipiki maarufu kama Bodaboda ambao wanafanya maandamano kuelekea kituo cha polisi kushinikiza wenzao wanaoshikiliwa waachiwe huru.

Hali hiyo imeanza majira ya saa sita mchana baada ya kile wanachodai kuwa askari wa usalama barabarani tangu asubuhi  wamekuwa wakikamata bodaboda na kasha kuwapiga bila makosa.

Barabara kuu ya mjini Kasulu itokayo maeneo ya makaburini hadi kituo cha polisi imefurika pikipiki zinazoendeshwa kwa fujo kuelekea mtaa wa mlimani kwa ajili ya kushinikiza polisi kuwaachia wenzao waliokamatwa

Hata hivyo habari zinaeleza kuwa, mtu mmoja leo amegongwa nagari eneo la soko kuu kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni msongamano wa pikipiki zinazopaki katika makutano ya barabara hali inayosababisha upishanaji wa watembea kwa miguu, magari na pikipiki kuwa wa shida.

Mzee huyo ambaye jina lake hadi sasa halijajulikana amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kasulu.
Share this article :
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377