Home » » WAKAZI ZAIDI YA MILIONI MOJA MKOANI GEITA HATARINI

WAKAZI ZAIDI YA MILIONI MOJA MKOANI GEITA HATARINI

Written By Unknown on Jumamosi, 26 Julai 2014 | 11:44



Sehemu ya kijiji cha Mwasabuka wilayani Nyang'hwale mkoani Geita ilivyoharibiwa kutokana na uchimbaji wa Dhahabu, Nyumba zaidi ya 500 hatarini kutokana na kuathiriwa na milipuko ya fataki za kuvunja miamba ya madini hayo

Asasi ya Okoa Mazingira REMA iliyoko mkoani Geita imeitaka serikali kufanya uchunguzi wa athari za mazingira zinazotokana na uchimbaji mkubwa na mdogo wa madini ya dhahabu mkoani humo ili kunusuru maisha ya wananchi

Rai hiyo imetolewa na katibu mtendaji wa asasi hiyo Bw. Idd Malangula wakati akiongea na Uhuru FM kuhusu athari za mazingira katika eneo la migodi ukanda wa ziwa Victoria

BW. Malangula  amebainisha kuwa asasi hiyo imebeini kuwepo kwa athari kubwa za kimazingira zinazotokana na makampuni ya madini kutozingatia hifadhi kanuni, pamoja na wachimbaji wadogo kutokuwa na elimu.

Amebainisha kuwa wananchi wanaopakana na migodi ya dhahabu mkoani Geita wako katika hatari ya kupoteza maisha kwa kuugua maradhi yanayotokana na matumizi ya maji yaliyochafuriwa na kemikali hatari kutoka migodini

Aidha Bw. Malangula ametaja kuwa utafiti uliofanywa na asasi yake katika bonde la mto Nyakabare wilayani Geita umebaini kuwepo kwa kemikali za baruti, vumbi na viwatilifu hatari ambavyo huenda vikawadhuru binadamu.

Nyakabare ni mto pekee ambao unategemewa na wakazi wa vijiji zaidi ya kumi na vine ambapo maji yake hutumika kwa matumizi ya nyumbani, kilimo na mazingira na maji yake huelekea ziwa Victoria.

Bw. Malangula amebainisha kuwa licha ya makampuni ya madini kutambua athari ya kimazingira na afya kwa binadamu, wameendelea kulipua baruti na kutumia kemikari ambazo kuishia katika mto huo jambo ambalo ni hatari kwa binadamu

Asasi ya REMA inayojishughulisha na hifadhi ya mazingira mkoani Geita ni moja ya makundi ambayo yanapigwa vita na na vikundi vya wachimbaji wadogo, wakubwa na taasisi za umma ambazo zinahusika na uharibifu huo wa mazingira,
Share this article :
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377