Home » » MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA

MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA

Written By Unknown on Alhamisi, 26 Juni 2014 | 14:55

Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria Kongamano la maadili lililoandaliwa na Baraza la habari Tanzania MCT mjini Bagamoyo.



Imeelezwa kuwa maslahi duni ya wafanyakazi wa vyombo vya habari kunatokana na kutokuwepo na chama cha wafanyakazi wa tasnia ya habari

Hayo yamebainishwa na katibu mtendaji wa Baraza la habari Tanzania Bw. Kajubi Mukajanga wakati akihitimisha kongamano la maadili ya uandishi wa habari mjini Bagamoyo leo.

Bw. Mukajanga amebainisha kuwa vyombo vingi vya habari haviwalipi ipasavyo watumishi wake na huchangia uandishi wa habari zisizozingatia weledi

Aidha amepongeza kuwepo mchakato wa kuanzisha chama cha wafanyakazi wa tasnia ya habari JUT na kuwahimiza waandishi wa habari kujiunga ili kuwa na nguvu.
Share this article :
 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377