HABARI MPYA
blink

UMOJA WA WAZAZI WAAZIMIA KUANZISHA SHULE KILA KATA

Written By Unknown on Alhamisi, 5 Juni 2014 | 05:47


Umoja wa wazazi wilaya ya Kasulu umeazimia kuanzisha shule za awali kila kata pamoja na vyama vya akiba na mikopo kwa dhamira ya kuinua kiwango cha ufahamu wa mabadiliko ya kimaisha pamoja na kipato cha kaya na kuepuka Rushwa nyakati za uchaguzi.

Imeelezwa kuwa uwepo wa vitendo vya rushwa katika chaguzi  mbalimbali kunatokana na jamii kutokuwa na elimu ya kutosha pamoja na umasikini ambao hutumiwa na wagombea kulaghai ili kupata kura

Umoja huo unaeleza kuamini kuwa endapo mfumo wa elimu za awali utaanzishwa katika ngazi cha chini pamoja na wazazi au kaya kuwa na kipato cha kutosha upo uwezekano wa wazazi kuwa na uwezo wa kupinga tabia za wanasiasa kuitumia fursa ya ujinga na umasikini kama chambo.

BODA BODA WAIIJIA JUU SERIKALI -WADAI ULINZI ZAIDI

Baadhi ya boda boda zikiwa nje ya ofisi ya CCm kasulu kulalamikia unyanyasaji





Umoja wa vijana wa CCM wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma umemtaka mkuu wa wilaya ya Kasulu kuitisha kikao cha kamati ya ulinzi na usalama kujadili mgogoro uliopo baina ya jeshi la polisi na vijana waendesha bodaboda.

Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa vijana wilaya Bw. Mberwa Chidebwe katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana mjini Kasulu kujadili mchakato wa katiba mpya

Bw. Mberwa ameeleza kuwa, waendesha pikipiki maarufu kama boda boda wamelalamikia kuwepo kwa uonevu na uvunjwaji wa sheria za usalama barabarani ambao hutekelezwa na baadhi ya askari wa jeshi la polisi

Ametaja uonevu huo kuwa ni kukamatwa hovyo na kuombwa Rushwa, kuzushiwa kesi za uongo, kuwekwa rumande kwa uda mrefu bila mashtaka na idara ya mahakama kuwahukumu kifungo kinyume cha sheria za usalama barabarani

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Dani Makanga amekiri kupokea malalamiko hayo na kuahidi kuchukua hatua ili kutatua mgogoro huo

WANAHABARI TANZANIA WAKUMBUSHWA KUUNGANA - IFJ


Mr. Louis Thomas - officer from International Federation for Journalists - IFJ addressing the Tanzania journalists during the seminar on crating a journalists union in Tanzania


Dar es salaam
By. Prosper Kwigize

Waandishi wa habari nchini Tanzania wamehimizwa kuungana na kutambua haki zao ili kujiendeleza kitaaluma na kimaslahi.

Rai hiyo imetolewa na afisa kutoka jumuiya ya kimataifa ya waandishi wa habari IFJ Bw. Louis Thomas wakati akitoa ujumbe wa umuhimu wa vyama vya wafanyakazi wa tasnia ya habari katika kikao cha wanahabari nchini jijini Dar es salaam leo.

Bw. Thomas amebainisha kuwa, malipo madogo yasiyolinganga na thamani ya taaluma katika nchini nyingi za afrika kunatokana na wanahabari wenyewe kutotambua wajibu na haki zao katika jamii.

Amesisitiza kuwa kuundwa kwa chama cha wafanyakazi wa sekta ya habari kutawasaidia waandishi na watumishi wa vyombo vya habari kudai na kupata haki za msingi kulingana na weledi wao.

Hata hivyo IFJ imeonya kuwepo kwa baadhi ya waandishi wa habari wasio na ujuzi ambao huharibu wasifu wa taaluma hiyo.

BURUANI KATIKA FILAMU- MFAHAMU JET LI

Written By Unknown on Alhamisi, 24 Aprili 2014 | 06:32

Jet Li
Li Lianjie (amezaliwa tar. 26 Aprili 1963) ni mshindi wa Tuzo za Filamu za Hong Kongo, akiwa kama mwigizaji bora filamu wa Kichina. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Jet Li. Jet Li ni mtaalam wa Kung Fu na Wushu. Baada ya miaka mitatu ya mafunzo ya Wushu, Jet Li alipata ushindi wake wa kwanza katika mashindano ya kitaifa ya vikosi vya Wushu kwa mji wa Beijing. Akiwa na umri wa miaka 17, Jet Li aliachana na masuala ya Uwushu na badala yake akaja kuwa mwigizaji wa filamu na akabahatika kutoa filamu yake kwanza mnamo mwaka wa 1982 na filamu ilikwenda kwa jina la Shaolin Temple. Badala ya hapo akawa anaendelea zaidi na maswala ya filamu na hata kuweza kujulikana katika medani hiyo ya uigizaji wa filamu katika China. Akaja kujipatia umaarufu zaidi pale alipocheza katika mfululizo wa filamu za Once Upon a Time in China, ambamo humo alikuwa akicheza kama shujaa wa kiasili - Wong Fei Hung. Kwa upande wa Marekani, Jet Li alianza kucheza kama adui katika filamu ya Lethal Weapon 4 kunako mwaka wa 1998, na kwa upande wa filamu alizocheza Marekani kwa mara ya kwanza na kuwa kama nyota kiongozi ilikuwa katika Romeo Must Die ya mwaka wa 2000. TANZAMA MOVIE ZAKE HAPA

HOTUBA YA RAIS KIKWETE NA JAJI WARIOBA -BUNGE LA KATIBA

Written By Unknown on Jumatatu, 21 Aprili 2014 | 05:02




 chanzo: youtube: Husein Hassan

HOTUBA ZA VIONGOZI KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA MPYA NCHINI TANZANIA NI MOJA YA MAMBO MUHIMU YANAYOTAKIWA KUSIKILIZWA NA WAJUMBE WAJIPE MUDA NA NAFASI YA KUTAFAKARI.

HII NI KUTOKANA NAUKWELI KWAMBA KUMEKUWA NA MIVUTANO KUTOKA KWA MAKUNDI YANAYOKINZANA KIFIKIRA, KIMLENGO NA KIMTAZAMO BILA KUSAHAU ITIKATI ZA KISIASA

KWA KUTAMBUA HAYO UKURASA HUU UNAKULETEA HOTUBA HIZO

Chanzo: MCL

WEMA SEPETU KUMVAA MRISHO NGASA LEO UWANJA WA TAIFA

Written By Unknown on Jumamosi, 19 Aprili 2014 | 06:55

http://kwigizenews.blogspot.nl/2014/04/wema-sepetu-kumvaa-mrisho-ngasa-leo.html


Katika hali inayovuta hisia za wengi, leo msanii maarufu ambaye pia amewahi kuwa miss Tanzania ametangaza kumfuata Mchezaji maarufu anayetajwa kuhama timu za Bongo kuliko wengine Mrisho Ngasa uwajani

Akiongea na vyombo vya habari Wema ametaja kuwa hana tabia ya kwenda kutazama mechi lakini leo atashuhudia mtanange baiana ya Simba na yanga ili baada ya mechi akutane na ngasa na kudai deni lake


Waswahili wanasema, “Ahadi ni Deni”, Wema anataja kuwa anamdai Ngassa ahadi ya mpira.

 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377