HABARI MPYA
blink
13:21
Zaidi ya watu 399 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya kuugua ugonjwa hatari wa Ebola katika nchi kadhaa za afrika magharibi.
Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO zilizokaririwa na mtandao wa PLEN MEDIA zaidi wa watu 635 wameambukizwa na kuugua ugonjwa huo unaoua haraka kuliko ugonjwa mwingine duniani.
WHO imetaja akuwa wengi kati ya waliofariki ni raia wa Liberia na Siera Lione na kwamba tahadhari zimechukuliwa zaidi ili kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo katika nchi jirani.
Ameongeza kuwa hawezi kusema kuwa wameshindwa kudhibiti lakini udharula wa mlipuko huo umeamsha mamlaka za ulinzi wa afya ya jamii kuchukua hatua za dharuala kuokoa wagonjwa na kuzuia maambukizi zaidi.
Kiasi cha maafisa wa WHO 150 wako katika maeneo yaliyoathiriwa na Ebola wakishirikiana na wizara za afya katika nchi hizo, vituo vya afya na klinic za jamii pamoja na wadau wengine wa afya wa kimataifa kutoa matibabu na kinga.
WHO mwishoni mwa wiki imekutana na wadau wa afya kutoka nchi 11 za ukanda wa magharibi ambapo walikutana katika nchi ya Ghana na kujadili juu ya mlipuko huo na namna nchi za ukanda huo zinavyopaswa kulichukulia tukio hilo kwa namna ya pekee ili kunusuru vifo zaidi
Kwa habari zaidi bofya hapa ebola Africa
399 WAMEPOTEZA MAISHA KWA UGONJWA WA EBOLA
Written By Unknown on Jumapili, 29 Juni 2014 | 13:21
![]() |
| Baadhi ya dalili za ugonjwa wa Ebola ni kutokwa damu mwilini, mdomoni, puani,machoni nk |
Zaidi ya watu 399 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya kuugua ugonjwa hatari wa Ebola katika nchi kadhaa za afrika magharibi.
Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO zilizokaririwa na mtandao wa PLEN MEDIA zaidi wa watu 635 wameambukizwa na kuugua ugonjwa huo unaoua haraka kuliko ugonjwa mwingine duniani.
WHO imetaja akuwa wengi kati ya waliofariki ni raia wa Liberia na Siera Lione na kwamba tahadhari zimechukuliwa zaidi ili kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo katika nchi jirani.
"Ni mlipuko wa hatari sana kuwahi kutokea katika ukanda huu" alisema Bw. Daniel Epstein, msemaji wa Shirika la Afya Duniani WHO.
Ameongeza kuwa hawezi kusema kuwa wameshindwa kudhibiti lakini udharula wa mlipuko huo umeamsha mamlaka za ulinzi wa afya ya jamii kuchukua hatua za dharuala kuokoa wagonjwa na kuzuia maambukizi zaidi.
Kiasi cha maafisa wa WHO 150 wako katika maeneo yaliyoathiriwa na Ebola wakishirikiana na wizara za afya katika nchi hizo, vituo vya afya na klinic za jamii pamoja na wadau wengine wa afya wa kimataifa kutoa matibabu na kinga.
WHO mwishoni mwa wiki imekutana na wadau wa afya kutoka nchi 11 za ukanda wa magharibi ambapo walikutana katika nchi ya Ghana na kujadili juu ya mlipuko huo na namna nchi za ukanda huo zinavyopaswa kulichukulia tukio hilo kwa namna ya pekee ili kunusuru vifo zaidi
Kwa habari zaidi bofya hapa ebola Africa
14:55
MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA
Written By Unknown on Alhamisi, 26 Juni 2014 | 14:55
![]() |
| Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria Kongamano la maadili lililoandaliwa na Baraza la habari Tanzania MCT mjini Bagamoyo. |
Imeelezwa kuwa maslahi duni ya wafanyakazi wa vyombo vya
habari kunatokana na kutokuwepo na chama cha wafanyakazi wa tasnia ya habari
Hayo yamebainishwa na katibu mtendaji wa Baraza la habari
Tanzania Bw. Kajubi Mukajanga wakati akihitimisha kongamano la maadili ya
uandishi wa habari mjini Bagamoyo leo.
Bw. Mukajanga amebainisha kuwa vyombo vingi vya habari haviwalipi
ipasavyo watumishi wake na huchangia uandishi wa habari zisizozingatia weledi
Aidha amepongeza kuwepo mchakato wa kuanzisha chama cha
wafanyakazi wa tasnia ya habari JUT na kuwahimiza waandishi wa habari kujiunga
ili kuwa na nguvu.
Labels:
Development stories
14:47
KIGOMA KUANZISHA BENKI YA MATOFARI
![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kanali mstaafu Issa Machibya |
Mkuu wa mkoa wa Kigoma kanali mstaafu Issa Machibya
amewataka viongozi wa umma kuhakikisha wanasimamia ipasavyo utekelezaji wa
ilani ya uchaguzi ili kuwaondoa wananchi katika lindi la umasikini.
Agizo hilo amelitoa wilayani Kibondo mkoni humo jana katika
ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo
Kanali Machibya amebainisha kuwa, kipimo cha utumishi ni
uadilifu na usimamizi mahili wa miradi ya maendeleo na kwamba wananchi wakipewa
hamasa na viongizi wao, watashiriki kikamilifu kutekeleza miradi yao
Aidha mkuu huyo wa mkoa ameanzisha kampeni maalumu ya
ufyatuaji na uchomaji wa matofali katika kila kijiji mkoani humo kwa lengo la
kuwa na benki ya matofari
Kanali Machibya amebainisha kuwa matofari licha ya kutumika
kujengea miundo mbinu ya huduma za jamii, pia ni chanzo cha mapato kwa vijana
mkoani Kigoma
Mkuu wa mkoa wa Kigoma alikuwa wilayani Kibondo kwa ziara ya
kikazi.
08:59






